Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 19 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 220 | 2026-04-29 |
Name
Abdallah Jafari Chaurembo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbagala
Primary Question
MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Charambe Magengeni hadi Zahanati ya Kilamba ili kuondoa kero kwa Wagonjwa wanaoenda Hospitali ya Wilaya?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge Jimbo la Chamazi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Charambe Magengeni hadi Zahanati ya Charambe (Kilamba) ina urefu wa kilometa 1.3, ambapo hadi sasa mita 590 zimeboreshwa kwa kiwango cha zege na ziko katika hali nzuri kwa gharama ya shilingi milioni 676.9 huku meta 710 zilizobaki bado ni za changarawe.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imepanga kuendelea kuijenga barabara hii kwa tabaka la zege kwa awamu na imeweka katika mpango na bajeti ya mwaka 2026/2027 kwa kutumia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Manispaa Temeke. Kiasi cha shilingi milioni 575.9 ambapo barabara hiyo itajengwa kwa urefu wa meta 710. Aidha, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa awamu katika bajeti ili kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved