Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 19 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 225 2026-04-29

Name

Amina Mussa Mkumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. AMINA M. MKUMBA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA katika Jimbo la Kibiti?

Name

Wanu Hafidh Ameir

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Mussa Mkumba, Mbunge wa Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Ujenzi wa Chuo cha VETA cha Wilaya ya Kibiti ni miongoni mwa ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi 65 vinavyoendelea kujengwa katika wilaya 64 na Mkoa mmoja wa Songwe. Ujenzi huo unafanyika katika wilaya au mkoa ambao hauna Chuo cha VETA.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na ujenzi wa Chuo cha VETA cha Wilaya ya Kibiti ambacho kinatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2026. Hadi sasa Serikali imeshatumia jumla ya shilingi bilioni 1.1 kati ya shilingi bilioni 1.6 zilizotengwa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa awamu ya kwanza. Mpaka sasa ujenzi huo umefikia 69% ya utekelezaji wake.