Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 19 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 226 | 2026-04-29 |
Name
Alan Thomas Mvano
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kakonko
Primary Question
MHE. ALAN T. MVANO aliuliza: -
Je, lini Mkandarasi atakamilisha kuchimba na kujenga kisima cha maji katika Kijiji cha Kihomoka kama ilivyo kwenye mkataba wake?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Alan Thomas Mvano, Mbunge wa Jimbo la Kakonko, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilipanga kuchimba visima vitano katika Wilaya ya Kakonko kupitia programu maalumu ya uchimbaji wa visima 900. Hadi sasa jumla ya visima vinne kati ya vitano vimechimbwa katika Kijiji cha Ruhuru viwili, Kihomoka kimoja, na Nyamtukuza kisima kimoja, ambapo kwa pamoja vina uwezo wa kuzalisha jumla ya maji lita 55,500 kwa saa.
Mheshimiwa Naibu Spika, visima hivyo baada ya kupata maji vimeendelezwa kwa kujengewa miundombinu rahisi ya kutolea huduma kwa wananchi (point source) na vinaendelea kutoa huduma iliyokusudiwa kwa wakazi wa vijiji hivyo. Hata hivyo kisima kimoja kilichokuwa kimepangwa kuchimbwa katika Kitongoji cha Centre B kilichopo Kijiji cha Kihomoka hakikuweza kuchimbwa. Hivyo, Serikali imekiingiza kisima hicho kwenye mpango wa programu ya vijiji 1,575 visivyokuwa na huduma ya maji ambayo inaanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2026/2027.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved