Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 19 Water and Irrigation Wizara ya Maji 227 2026-04-29

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: -

Je, lini Mradi wa Maji katika Kijiji cha Mpandapanda, Kata ya Kiwira, utaanza kutekelezwa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kijiji cha Mpandapanda kilichopo Kata ya Kiwira kinapata huduma ya majisafi na salama kupitia mradi uliotekelezwa kijijini hapo mwaka 2021/2022 kupitia fedha za UVIKO 19. Kiasi cha shilingi milioni 306.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuboresha zaidi huduma ya maji Kata ya Kiwira, Serikali imekamilisha usanifu wa mradi mkubwa utakaotumia chanzo cha maji cha Mto Katalifu unaolenga kunufaisha vijiji vyote vinne vya Mpandapanda, Kikota, Ilundo na Ibula. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuanza utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 5.2.