Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 19 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 231 2026-04-29

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:-

Je, lini barabara ya Mlowo – Kamsamba itaanza kujengwa kwa kuwa ni zaidi ya mwaka tangu mkandarasi asaini mkataba?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mlowo - Kamsamba yenye urefu wa kilomita130 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha ambapo Serikali tayari imekamilisha ujenzi wa Daraja la Momba na Daraja la Mpapa. Aidha, Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa kilometa tano kuanzia Mlowo kuelekea Kamsamba na kilometa nyingine tano kuanzia Kamsamba kuelekea Mlowo amepatikana, ambapo taratibu za malipo ya awali ya kumwezesha kuanza kazi, zinaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sehemu zilizobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi.