Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 19 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 232 | 2026-04-29 |
Name
Asia Abdulkarim Halamga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanzisha kiwanda cha kuchakata mazao katika Jimbo la Hanang?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Abdulkarim Halamga, Mbunge wa Jimbo la Hanang kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Hanang huzalisha mazao mbalimbali ikiwemo mahindi, alizeti, ngano, dengu na mbaazi. Mwaka 2024/2025 wilaya hii ilizalisha mahindi tani 130,980.3, alizeti tani 30,732.3, mbaazi tani 19,173.6, dengu tani 30,960.2, na ngano tani 12,600. Wilaya hii ina jumla ya viwanda 1,226, ambapo kati ya hivyo viwanda vya kuchakata mahindi ni 346 na viwanda vya kukamua mafuta ya alizeti ni 69. Viwanda 811 vinavyobaki ni vya matofali, mbao, kushona na mikate.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Wizara ya Kilimo pamoja na Mkoa wa Manyara tunaendelea kutafuta wawekezaji kwa ajili ya kujenga viwanda vya mazao ya dengu, ngano na mbaazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved