Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 17 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 194 | 2026-04-27 |
Name
Juma Ramadhani Mustafa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Igalula
Primary Question
MHE. JUMA M. KAWAMBA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Shule za Msingi na Sekondari, pamoja na miundombinu katika Shule zilizopo Jimbo la Igalula?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Mustapha Kawamba, Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya vipaumbele vya Serikali katika sekta ya elimu msingi na sekondari ni pamoja na ujenzi wa madarasa, shule za msingi na sekondari katika maeneo mbalimbali yenye vigezo stahiki kote nchini. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 – 2025/2026 Serikali imetoa shilingi bilioni 4.23 katika jimbo la Igalula, kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili za msingi za Mnadani na Izumba Migusa, shule nne za sekondari za Venant Daud, Mmale, Magulyati na Uyui Modern na madarasa 33 katika shule 17 za msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2026/2027 Serikali imetenga shilingi bilioni 1.25 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Mzumba na madarasa 54, ya msingi 40 na ya sekondari 14, pamoja na matundu ya vyoo 10 katika shule mbili za sekondari. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule za msingi na sekondari na kuongeza miundombinu katika shule zilizopo kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved