Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 17 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 197 2026-04-27

Name

Eng. Johnston Johansen Mutasingwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Primary Question

MHE. ENG. JOHNSTON J. MUTASINGWA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha upanuzi wa Kituo cha umeme Kibeta?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Eng. Johnston Johansen Mutasingwa, Mbunge wa Bukoba Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa Serikali kupitia TANESCO inaendelea na upanuzi wa Kituo cha Kupooza Umeme cha Kibeta kwa kuongeza uwezo wa transfoma iliyokuwepo kutoka MVA 20 na kufunga transfoma yenye uwezo wa miundombinu ya Gridi ya Taifa ambapo utekelezaji wake umefikia 95% na unatarajiwa kukamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu wa 2026. Ahsante sana.