Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 18 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 203 | 2026-04-28 |
Name
John Francisco Nzilanyingi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nyamagana
Primary Question
MHE. JOHN F. NZILANYINGI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara za pembezoni na mtaani maeneo ya Kushiri, Mahina, Luchelele na Lwanchima?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa John Francisco Nzilanyingi, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea na utekelezaji wa miradi ya ujenzi na matengenezo ya mara kwa mara ya barabara za vijijini na mjini ili kuwezesha shughuli za usafirishaji kufanyika kwa urahisi kote nchini ikiwemo katika Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya fedha za barabara katika Jimbo la Nyamagana imeongezeka kutoka shilingi bilioni 3.47 mwaka 2020/2021 hadi shilingi bilioni 6.49 mwaka 2025/2026.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya barabara zinazoendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sasa katika Jimbo la Nyamagana ni pamoja na ujenzi wa barabara ya Mwananchi - Mahinakati kilometa 0.3, Mwananchi - Bugurika kilometa 0.16, Igelegele - Mahinakati, Buhongwa - Lwanchima (kilometa 3.8) ambazo kwa pamoja zinagharamia jumla ya takribani shilingi milioni 853.28. Aidha, ujenzi wa barabara ya Buhongwa - Lwanchima (kilometa 3.8) umetekelezwa kwa shilingi bilioni 5.9 kupitia mradi wa TACTIC.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia bajeti ya mwaka 2024/2025 Serikali imeendelea na ujenzi wa barabara ya Kishiri - Fumagila (kilometa 1.5) kwa shilingi milioni 304.99 na katika mwaka wa fedha 2026/2027 zimetengwa fedha kiasi cha shilingi milioni 83.93 ujenzi wa barabara ya Bugayamba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti ya kujenga barabara za pembezoni kwa awamu katika Jimbo la Nyamagana zikiwemo barabara za Kushiri, Mahina, Luchelele na Lwanchima. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved