Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 203 2026-04-28

Name

John Francisco Nzilanyingi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question


MHE. JOHN F. NZILANYINGI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara za pembezoni na mtaani maeneo ya Kushiri, Mahina, Luchelele na Lwanchima?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa John Francisco Nzilanyingi, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea na utekelezaji wa miradi ya ujenzi na matengenezo ya mara kwa mara ya barabara za vijijini na mjini ili kuwezesha shughuli za usafirishaji kufanyika kwa urahisi kote nchini ikiwemo katika Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya fedha za barabara katika Jimbo la Nyamagana imeongezeka kutoka shilingi bilioni 3.47 mwaka 2020/2021 hadi shilingi bilioni 6.49 mwaka 2025/2026.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya barabara zinazoendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sasa katika Jimbo la Nyamagana ni pamoja na ujenzi wa barabara ya Mwananchi - Mahinakati kilometa 0.3, Mwananchi - Bugurika kilometa 0.16, Igelegele - Mahinakati, Buhongwa - Lwanchima (kilometa 3.8) ambazo kwa pamoja zinagharamia jumla ya takribani shilingi milioni 853.28. Aidha, ujenzi wa barabara ya Buhongwa - Lwanchima (kilometa 3.8) umetekelezwa kwa shilingi bilioni 5.9 kupitia mradi wa TACTIC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia bajeti ya mwaka 2024/2025 Serikali imeendelea na ujenzi wa barabara ya Kishiri - Fumagila (kilometa 1.5) kwa shilingi milioni 304.99 na katika mwaka wa fedha 2026/2027 zimetengwa fedha kiasi cha shilingi milioni 83.93 ujenzi wa barabara ya Bugayamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti ya kujenga barabara za pembezoni kwa awamu katika Jimbo la Nyamagana zikiwemo barabara za Kushiri, Mahina, Luchelele na Lwanchima. Ahsante.