Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 204 2026-04-28

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-

Je, lini Serikali itakarabati Shule ya Msingi Mtapenda Kata ya Mtapenda – Nsimbo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Jimbo la Nsimbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Msingi Mtapenda ilijengwa mwaka 1970, na hivyo ni chakavu na inahitaji ukarabati. Katika mipango ya ukarabati wa shule chakavu, Serikali katika mwaka 2021/2022 ilifanya tathmini na kubaini jumla ya shule 10,595 chakavu kote nchini ambapo jumla ya shilingi trilioni 2.8 zinahitajika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kuptia Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, imeandaa andiko la mradi unaoitwa SIFA yaani (School Infrastructure Facelifting Programme) na kuwasilisha Wizara ya Mipango na Uwekezaji ili kuwezesha upatikanaji wa fedha za kufanyia ukarabati wa shule zote kongwe za awali, msingi na Sekondari nchini ikiwemo Shule ya Msingi Mtapenda, ahsante.