Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 18 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 207 | 2026-04-28 |
Name
Saashisha Elinikyo Mafuwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Hai
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kada ambazo hazipo kwenye orodha ya kada za Sekretarieti ya Ajira kwa kuwa zinafundishwa vyuoni?
Name
Regina Ndege Qwaray
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kuwa vyuo Vikuu na vyuo vya elimu ya juu hutoa mafunzo ya programu za fani mbalimbali kwa vijana ambao wanaweza kuajiriwa katika utumishi wa umma au katika sekta binafsi nchini. Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma husimamia taratibu za ajira kwa kuzingatia sifa zilizoainishwa katika miundo ya maendeleo ya utumishi ya kada zilizo chini ya Wizara mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kuwa baadhi ya fani zinazofundishwa katika vyuo vikuu na vyuo vya elimu ya juu hazijawekewa utaratibu wa ajira kama fani nyingine ambazo wahitimu wake wanaajiriwa katika utumishi wa umma au sekta binafsi. Hivyo, tunaelekeza vyuo kuwasiliana na Serikali mapema kabla ya kuanzisha programu za fani ili kuwezesha utengenezaji wa mifumo ya ajira hizo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved