Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 18 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishat | 208 | 2026-04-28 |
Name
Nape Moses Nnauye
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtama
Primary Question
MHE. NAPE M. NNAUYE aliuliza: -
Je, Serikali ipo tayari kuweka wazi mpangokazi wa mwelekeo wa mazungumzo juu ya Mradi wa LNG - Lindi kwa kuwa umechukua muda mrefu?
Name
Deogratius John Ndejembi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chamwino
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Nape Moses Nnauye, Mbunge wa Jimbo la Mtama, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali na wawekezaji wa mradi wa LNG wapo katika hatua ya mwisho ya majadiliano hususani kwenye masuala ya kisheria ili kuwezesha usainishaji wa mikataba na makubaliano na hatimaye utekelezaji wa mradi kuanza. Aidha, majadiliano yatakapokamilika, rasimu za mikataba hiyo zitawasilishwa Serikalini kwa ajili ya mapitio na kupata ridhaa kabla ya kusainiwa rasmi ili kuwezesha utekelezaji wa Mradi kuanza mara moja.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved