Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 18 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 209 | 2026-04-28 |
Name
Innocent Lugha Bashungwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karagwe
Primary Question
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Umeme katika Shule za Sekondari, Msingi na Taasisi zote za Wilaya ya Karagwe?
Name
Deogratius John Ndejembi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chamwino
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Lugha Bashungwa, Mbunge wa Jimbo la Karagwe kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Karagwe jumla ya vitongoji 334 kati ya vitongoji 612 vimepatiwa umeme hadi sasa na Shule za Msingi 109, Shule za Sekondari 37 za vitongoji hivyo zimeunganishiwa umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakandarasi wanaendelea na utekelezaji wa mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 61 ambapo kipaumbele ni kufikisha umeme katika taasisi zinazohudumia jamii zikiwemo shule, vituo vya afya, pampu za maji na nyumba za ibada. Aidha, Serikali itaendelea kuziunganishia umeme taasisi katika vitongoji 217 vya Wilaya ya Karagwe vilivyosalia kupitia miradi mbalimbali ya umeme inayotarajia kuanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2026/2027.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved