Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 18 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 210 2026-04-28

Name

Kassimu Amari Mbaraka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. KASSIMU A. MBARAKA aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa Barabara ya Kiomoni, Pande, Mjesani hadi Muheza inayounganisha Wilaya ya Tanga na Muheza utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Kassimu Amari Mbaraka, Mbunge wa Tanga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kiomoni, Pande, Mjesani ni sehemu ya barabara ya Mkoa ya Mlingano – Mjesani - Pande hadi Kiomoni yenye urefu wa kilometa 39.5 na inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS). Kazi ya upembuzi yakinifu na Usanifu wa Kina wa barabara hii kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami inaendelea na inatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2027. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.