Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 18 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 211 2026-04-28

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kilometa 23 kutoka Mlandizi hadi Ruvu Station (SGR) kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mlandizi hadi Stesheni ya SGR kilometa 23 inaunganisha barabara ya Morogoro (TANZAM) katika eneo la Mlandizi na Reli ya SGR katika Stesheni ya Ruvu. Kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, tayari Serikali imesaini mkataba na Mkandarasi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hiyo, na kwa sasa, Serikali inaendelea na taratibu za malipo ya awali ili kumwezesha Mkandarasi kuanza kazi za ujenzi.