Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kilometa 23 kutoka Mlandizi hadi Ruvu Station (SGR) kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii inaungana na Barabara ya Tanga – Segera - Dar es Salaam na Barabara ya Dar es Salaam – Segera – Moshi - Arusha ambayo kwa sasa imezidiwa na magari mengi hasa malori kutoka Bandari ya Tanga. Je, ni upi mkakati wa upanuzi wa barabara hii pamoja na barabara ambayo Mheshimiwa Hawa ameuliza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge kwamba hizi barabara nyingi zimechoka, lakini pia zimekuwa finyu. Mkakati ambao tunao, kwanza kuanzia Mlandizi hadi Chalinze ni kuweka expressway ambazo zitakuwa ni njia nne, lakini kuanzia Mlandizi kwenda Segera tulishafanya usanifu ili kuweza kuongeza upana wa hiyo barabara na kuweza kwenda na upana wa barabara ambazo sasa hivi zinajengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua ni barabara ambayo imejengwa muda mrefu, na kwa kweli ni finyu hasa kulingana na kazi kubwa ambayo imefanyika kuipanua Bandari ya Tanga na kuongeza mizigo na kufanya magari yawe mengi. Kwa hiyo, tuko na mpango wa kuweza kuipanua hiyo barabara.