Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 17 Water and Irrigation Wizara ya Maji 199 2026-04-27

Name

Yagi Maulid Kiaratu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. YAGI M. KIARATU aliuliza: -

Je, lini mradi wa maji unaotekelezwa katika mitaa 38 ya Manispaa ya Singida utakamilika ili wananchi wapate huduma ya majisafi na salama?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yagi Maulid Kiaratu, Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maji wa mitaa 88 katika Manispaa ya Singida ni miongoni mwa Mradi wa Maji wa Miji 28 unaotekelezwa na Serikali kwa gharama ya Dola za Kimarekani milioni 17.7. Kazi zilizopangwa kutekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na uchimbaji wa visima virefu 12, ujenzi wa matanki tisa yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 4.1, ulazaji wa mabomba umbali wa kilomita 58.7 sanjari na ujenzi wa kituo cha uendeshaji wa mitambo (pump station).

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa miundombinu mingine unaendelea sambamba na utafiti wa maji chini ya ardhi ili kuweza kupata visima vitakavyoweza kukidhi mahitaji ya mradi huu ambayo ni lita za maji milioni 22.3 kwa siku. Aidha, visima vitatu tayari vimechimbwa na vina uwezo wa uzalishaji wa maji zaidi ya lita milioni 4.9 kwa siku. Mpango wa Serikali ni kuhakikisha visima vyote vinavyohitajika vinachimbwa na mradi kuendelea na utekelezaji ambapo unatarajiwa, kwa mujibu wa mkataba, utakamalika ndani ya mwaka wa fedha 2026/2027.