Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 17 Water and Irrigation Wizara ya Maji 200 2026-04-27

Name

Esther Nicholas Matiko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, lini Mradi wa Maji Ziwa Victoria utakamilika na kutoa huduma ya Maji kwa Mitaa yote 81 ndani ya Mji wa Tarime?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa Maji wa Miji 28 wa Rorya - Tarime uliopo mkoani Mara kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 134. Kazi zinazotekelezwa kupitia mradi huu ni pamoja na ujenzi wa dakio (intake) katika Ziwa Victoria lenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 29 kwa siku; ujenzi wa mtambo wa kutibu maji, (treatment plant), wenye uwezo wa kutibu maji lita milioni 28 kwa siku; ulazaji wa mabomba umbali wa kilomita 110; ujenzi wa matanki matatu yenye jumla ya ujazo wa lita milioni kumi; sanjari na ujenzi wa kituo kimoja cha kusukuma maji, (booster station).

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi huu umefikia wastani wa 16% na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka wa fedha 2026/2027 kulingana na upatikanaji wa fedha, ambapo unalenga kunufaisha zaidi ya wananchi 460,000 waishio katika Wilaya za Rorya na Tarime, ikiwemo mitaa 81 iliyopo kwenye kata nane za Tarime Mjini.