Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 17 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 202 | 2026-04-27 |
Name
Enock Zadock Koola
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Vunjo
Primary Question
MHE. ENOCK Z. KOOLA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanzisha Kituo cha kukodi vifaa vya kilimo katika Wilaya ya Moshi Vijijini?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo inaendelea kutekeleza mpango wa uanzishaji wa vituo 1,000 vya kutoa huduma ya zana za kilimo kwa wakulima katika ngazi ya Kata ifikapo mwaka 2030, lengo likiwa ni kusogeza na kuwawezesha wakulima, kupata huduma za zana za kilimo kwa wakati na gharama nafuu ili kuongeza uzalishaji na tija.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza hilo, Wizara imeanzisha vituo 79 katika Halmashauri mbalimbali nchini, ikiwemo Halmashauri ya Moshi ambapo jumla ya matrekta madogo ya mkono (Power tiller) 29 na zana zake zimepelekwa ili kutoa huduma ya zana za kilimo kwa wakulima wa maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kufungua vituo vya zana za kilimo nchini ikiwemo Wilaya ya Moshi vijijini kwa kuzingatia mahitaji yaliyopo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved