Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 18 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 214 | 2026-04-28 |
Name
Ester Edwin Malleko
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza skimu za umwagiliaji katika Mkoa wa Kilimanjaro?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Maleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuchukua jitihada mbalimbali za kuendeleza sekta ya umwagiliaji nchini ikiwemo katika Mkoa wa Kilimanjaro. Katika kutekeleza hilo, mwaka 2025/2026, miradi 42 ya umwagiliaji inatekelezwa katika Mkoa wa Kilimanjaro ikijumuisha ujenzi na ukarabati wa skimu 15 zenye jumla ya hekta 18,154.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya skimu hizo, skimu nane ni za ujenzi zenye jumla ya hekta 9,514 ambapo utekelazaji wake umefikia wastani wa 28%. Aidha, miradi ya ukarabati ni saba ambapo utekelezaji wake umefikia wastani wa 45%. Kukamilika kwa ujenzi na ukarabati wa miradi hiyo kutawezesha kumwagilia eneo lenye ukubwa wa hekta 18,154 na kunufaisha wakulima 283,877.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa miradi ikiwemo Bonde la Mtambo lenye miradi ya Kikavu chini, Mapacha, Mtambo, Ismail na Ngosero (Mpenda Roho na Longoi) yenye jumla ya hekta 8,500. Aidha, miradi 18 ya skimu zenye zaidi ya hekta 29,000 usanifu wake unaendelea.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved