Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 18 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 214 2026-04-28

Name

Ester Edwin Malleko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza skimu za umwagiliaji katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Maleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuchukua jitihada mbalimbali za kuendeleza sekta ya umwagiliaji nchini ikiwemo katika Mkoa wa Kilimanjaro. Katika kutekeleza hilo, mwaka 2025/2026, miradi 42 ya umwagiliaji inatekelezwa katika Mkoa wa Kilimanjaro ikijumuisha ujenzi na ukarabati wa skimu 15 zenye jumla ya hekta 18,154.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya skimu hizo, skimu nane ni za ujenzi zenye jumla ya hekta 9,514 ambapo utekelazaji wake umefikia wastani wa 28%. Aidha, miradi ya ukarabati ni saba ambapo utekelezaji wake umefikia wastani wa 45%. Kukamilika kwa ujenzi na ukarabati wa miradi hiyo kutawezesha kumwagilia eneo lenye ukubwa wa hekta 18,154 na kunufaisha wakulima 283,877.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa miradi ikiwemo Bonde la Mtambo lenye miradi ya Kikavu chini, Mapacha, Mtambo, Ismail na Ngosero (Mpenda Roho na Longoi) yenye jumla ya hekta 8,500. Aidha, miradi 18 ya skimu zenye zaidi ya hekta 29,000 usanifu wake unaendelea.