Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Edwin Malleko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza skimu za umwagiliaji katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa baadhi ya miradi iko kwenye wastani wa 28% na 45%, je, ni upi mkakati wa Serikali sasa kuhakikisha miradi hii inatekelezwa kwa kasi ili wananchi waweze kufaidika mapema?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Esther Maleko kwa swali zuri la msingi na kufuatilia wananchi wake wa mkoa mzima wa Kilimanjaro. Jambo moja ambalo ninaweza nikamthibitishia kwa 100% ni kwamba miradi hii itakamilika kama ambavyo imepangwa. Kwa kuwa Wizara ya Fedha, sasa hivi ilishaweka commitment ya kuipatia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kila mwezi shilingi bilioni 25 zitakazokwenda kwenye miradi ya umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, fedha hizo zitasaidia kusukuma hii miradi iweze kukamilika kwa wakati kwa sababu tutawalipa kwa wakati, na sisi tutawasimamia kuhakikisha miradi hii inaenda kwa kasi. Kwa hiyo, nimwondoe shaka Mheshimiwa Mbunge kwamba na sisi tuko katika area of comfort kwamba miradi hii inakwenda kukamilika, ahsante sana.