Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 18 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 215 | 2026-04-28 |
Name
Zuberi Yahya Mfaume
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini
Primary Question
MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:-
Je, lini wakulima wa ufuta wa Kisaki, Mvuha, Mngazi, Bwakila chini na Selembala waliouza kwa Mfumo wa Stakabadhi Ghalani watalipwa?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Yahya Mfaume, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika msimu wa mwaka 2024/2025, wakulima wa ufuta katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro waliuza jumla ya tani 3,984 zenye thamani ya shilingi bilioni 9.841 kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na minada ya kidijiti. Kati ya kiasi hicho, madai ya shilingi bilioni 8.469 yalilipwa kwa wakulima kupitia mfumo huo na shilingi bilioni 1.372 hazikulipwa kwa wakati kutokana na dosari mbalimbali katika mifumo ya malipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufikia mwezi Oktoba, 2025, madai yote ya wakulima waliouza ufuta kupitia mfumo huo yalilipwa kikamilifu katika maeneo ya Mngazi, Selembala, Bwakila Chini, Kisaki na Mvuha. Mfumo huo umeendelea kuongeza uwazi, kuondoa ucheleweshaji wa malipo na kuhakikisha wakulima wanapata stahiki zao kwa wakati. Aidha, Serikali inatoa wito endapo kuna Mkulima ana changamoto katika malipo yake, awasilishe madai yake ili yaweze kupatiwa ufumbuzi kwa mujibu wa taratibu zilizopo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved