Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 18 Water and Irrigation Wizara ya Maji 217 2026-04-28

Name

Fadhili Sandali Chilombe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Miradi ya Maji katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mhandisi Fadhili Sandali Chilombe, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa jumla ya miradi ya maji sita yenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 7.8 katika Wilaya ya Tunduru ikiwemo Jimbo la Tunduru Kusini mkoani Ruvuma. Baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na mradi wa Tuwemacho, Masuguru - Mchoteka Awamu I, Misechela - Liwanga, Msinjili na Azimio.

Zijin ya China Miradi hiyo inajumuisha ujenzi wa vyanzo vya maji, ujenzi wa matanki manne yenye ujazo wa lita 750,000, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 74.1 sanjari na ujenzi wa vituo 25 vya kuchotea maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshalipa jumla ya shilingi bilioni 2.9 kwa miradi hiyo ambapo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na inatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka wa fedha 2026/2027 kulingana na upatikanaji wa fedha.