Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 42 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 498 2026-06-03

Name

Mwamengo Ulimboka Baraka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. BARAKA A. U. MWAMENGO aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya Ipinda?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA, SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Baraka Ulimboka Mwamengo, Mbunge wa Jimbo la Kyela.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uhitaji mkubwa wa magari ya kubebea wagonjwa. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 hadi sasa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI imepokea jumla ya magari ya kubeba wagonjwa 382 na magari 212 ya uratibu na usimamizi wa shughuli za afya. Magari hayo yamepelekwa kwenye mikoa na halmashauri zote nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kyela ilipokea gari moja la uratibu na usimamizi wa shughuli za afya na magari mawili ya kubebea wagonjwa ambapo gari moja lipo Kituo cha Afya Kilasilo na lingine Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyela. Kwa sasa Kituo cha afya Ipinda kinahudumiwa na gari la wagonjwa lililopo Hospitali ya Wilaya ya Kyela.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili kuendelea kununua magari ya kubebea wagonjwa na kuyapeleka kwenye halmashauri zenye upungufu ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Kyela.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.