Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 42 | Water and Irrigation | Wizara ya Kilimo | 500 | 2026-06-03 |
Name
Abdallah Dadi Chikota
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nanyamba
Primary Question
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:-
Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Arusha Chini utaanza kujengwa?
Name
Daniel Godfrey Chongolo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Makambako
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umwagiliaji nchini ikiwemo katika Mkoa wa Mtwara. Lengo la utekelezaji wa miradi hiyo ni kuimarisha uzalishaji wa mazao ya kilimo na kuchangia kuongeza kipato cha wakulima kupitia kilimo cha umwagiliaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza hilo, hadi kufikia Machi, 2026 mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Arusha Chini amepatikana na kukabidhiwa eneo la mradi kwa ajili ya ujenzi. Mradi huo una ukubwa wa jumla ya hekta 264 ambapo gharama za utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo ni shilingi bilioni 14.83.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kukamilika kwa mradi huo kutanufaisha wakulima 950 katika Vijiji vya Arusha, Arusha Juu, Mkomo, Ngorongoro, Chawi, Chawi Sokoni, Mchanje na Ngonja na hivyo kuwezesha wakulima kulima zaidi ya mara mbili kwa mwaka.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved