Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 42 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 501 | 2026-06-03 |
Name
Eng. Ezra John Chiwelesa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Biharamulo Magharibi
Primary Question
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Wilaya Biharamulo ili kuwezesha vijana kujikwamua kutokana na mafunzo yanayotolewa?
Name
Wanu Hafidh Ameir
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia ninaomba kujibu swali namba 501 la Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha VETA cha Wilaya ya Biharamulo ni miongoni mwa vyuo 64 vya VETA vinavyojengwa na Serikali katika Mkoa na Wilaya ambazo hazina Vyuo vya Ufundi Stadi. Mradi huu unalenga kuongeza fursa za mafunzo na kusogeza huduma karibu na wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Chuo cha VETA cha Wilaya ya Biharamulo unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2026. Hadi sasa Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 1.12 kati ya shilingi bilioni 1.6 zilizotengwa kwa ajili ya kukamilisha awamu ya kwanza ya mradi huu na ujenzi wake umefikia 72%.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved