Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 42 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 502 2026-06-03

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa minara ya mawasiliano Halmashauri ya Mji Ifakara hasa Ikwambi, Mang’ula B na Kanyenja?

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Kilombero, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imeendelea kutekeleza miradi ya kuboresha Huduma za Mawasiliano katika Jimbo la Kilombero. Katika utekelezaji wa Awamu ya Kwanza ya Mradi wa Tanzania ya Kidijitali, mnara wa mawasiliano wa mtoa huduma Honora (Yas) ulijengwa Kata ya Signal katika Kijiji cha Sagamaganga na unatoa huduma katika Vijiji vya Signal, Sululu na Sagamaganga. Aidha, kupitia awamu hiyo Kampuni ya Honora ilijenga mnara katika Kijiji cha Mhelule, Kata ya Mang’ula, unaohudumia vijiji vya Kanyenja, Mhelule, Mikoleko, Mang’ula A na Mang’ula B.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mnamo tarehe 8 Aprili, 2026, UCSAF ilifanya tathmini katika Vijiji vya Mang’ula B, Kanyenja na Kitongoji cha Ikwambi na kubaini kuwa Kijiji cha Kanyenja kilijumuishwa katika Mradi wa Mawasiliano ya Simu vijijini wa minara 636 ambapo mnara huo ulijengwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika Kijiji cha Kanyenja na unatoa huduma za teknolojia ya 2G na 4G. Aidha, Kijiji cha Mang’ula B na Kitongoji cha Ikwambi vilibainika kuwa na changamoto za mawasiliano hivyo UCSAF itayajumuisha maeneo hayo kwenye miradi ya mawasiliano ya simu ya mwaka wa fedha 2026/2027 kwa lengo la kutatua changamoto zilizopo katika Kijiji cha Mang’ula B na Kitongoji cha Ikwambi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.