Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 42 Water and Irrigation Wizara ya Maji 503 2026-06-03

Name

Amosy William Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA aliuliza: -

Je, lini maji ya Ziwa Victoria yataanza kusambazwa katika Kata za Pangale, Mpombwe, Igigwa, Kisanga, Tutuo, Mkolye, Chabutwa na Ipoje?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mhandisi Amosy William Maganga, Mbunge wa Jimbo la Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Miji 28 kwa kutumia maji ya Ziwa Victoria kutoka Tabora kwenda katika Wilaya za Sikonge, Urambo na Kaliua mkoani Tabora kwa gharama ya shilingi bilioni 143.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa kazi zinazotekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 253 sambamba na ujenzi wa matanki tano yenye jumla ya ujazo wa lita milioni nane yakiwemo matanki mawili yenye ujazo wa lita milioni tatu yaliyojengwa katika maeneo ya Tumbili na Misheni, wilayani Sikonge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huo umefikia wastani wa 76.5% za utekelezaji na umeanza kutoa huduma kwenye baadhi ya maeneo ya Mji wa Sikonge wakati utekelezaji ukiendelea. Mradi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2026 ambapo Serikali itafanya usanifu wa kufikisha huduma ya maji kupitia mradi huo kwenye maeneo ya pembezoni umbali wa kilometa 12 kutoka bomba kuu ikiwemo Kata za Pangale, Mpombwe, Igigwa, Kisanga, Tutuo, Mkolye, Chabutwa na Ipoje.