Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 23 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 255 2026-05-06

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza utekelezaji wa Mradi wa TACTIC katika Jimbo la Bagamoyo baada ya usanifu kukamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo ni miongoni mwa miji 45 inayotekeleza Mradi wa TACTIC nchini wenye barabara zenye urefu wa jumla ya Kilometa 4.5 pamoja na ujenzi wa barabara hizo kwa kiwango cha lami. Mradi huu pia utahusisha ujenzi wa stendi kuu ya mabasi Bagamoyo katika Kata ya Nia Njema, eneo la Kichemchem.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kukamilisha usanifu wa miradi hii, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia inaendelea na taratibu za kifedha kabla ya kuanza utekelezaji wa Miradi katika kundi hili ukiwemo Mji wa Bagamoyo.