Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 23 | Union Affairs | Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano | 256 | 2026-05-06 |
Name
Haji Kombo Mdowe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nungwi
Primary Question
MHE. MDOWE HAJI KOMBO aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga ukuta katika Fukwe za Bahari ya Nungwi Kiungani ili kuzuia bahari kuingia katika makazi ya watu?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mdowe Haji Kombo, Mbunge wa Nungwi, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi ikiwemo mmonyoko wa fukwe unaosababisha bahari kuingia katika makazi ya wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza hili, Serikali imefanikiwa kupata ufadhili kupitia Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund) ambapo jumla ya dola za Marekani 500,000 sawa na takribani shilingi bilioni 1.3 za Kitanzania zimetolewa na mfuko husika kwa ajili ya kutekeleza mradi katika mwaka wa fedha 2025/2026 na 2026/2027 wa kuimarisha utayari wa Kisiwa cha Zanzibar kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Mradi huu utaanza mara baada ya tathmini ya athari hizo kukamilika. Ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved