Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 23 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 256 2026-05-06

Name

Haji Kombo Mdowe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. MDOWE HAJI KOMBO aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga ukuta katika Fukwe za Bahari ya Nungwi Kiungani ili kuzuia bahari kuingia katika makazi ya watu?

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mdowe Haji Kombo, Mbunge wa Nungwi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi ikiwemo mmonyoko wa fukwe unaosababisha bahari kuingia katika makazi ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza hili, Serikali imefanikiwa kupata ufadhili kupitia Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund) ambapo jumla ya dola za Marekani 500,000 sawa na takribani shilingi bilioni 1.3 za Kitanzania zimetolewa na mfuko husika kwa ajili ya kutekeleza mradi katika mwaka wa fedha 2025/2026 na 2026/2027 wa kuimarisha utayari wa Kisiwa cha Zanzibar kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Mradi huu utaanza mara baada ya tathmini ya athari hizo kukamilika. Ninaomba kuwasilisha.