Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 23 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 258 | 2026-05-06 |
Name
Mwamengo Ulimboka Baraka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kyela
Primary Question
MHE. BARAKA A. U. MWAMENGO aliuliza: -
Je, lini Barabara ya Ipyana – Kasumulu – Ileje itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Baraka Ulimboka Mwamengo, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Ipyana – Kasumulu – Ngana – Ndembo – Ileje eneo la Isongole lenye urefu wa kilometa 114.3 ambapo kwa sasa kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii imefikia 96%. Aidha, Serikali imeanza ujenzi wa barabara hii sehemu ya Isongole II – Ndembo pamoja na barabara ya kuingia Ndembo – Isoko yenye urefu wa kilometa 52 ambapo ujenzi umefikia 10.75%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sehemu ya Ipyana – Kasumulu – Ngana hadi Ndembo kazi ya kufanya uthamini wa nyumba na mali kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi watakaoathiriwa na mradi huo inategemea kuanza hivi karibuni.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved