Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 23 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 258 2026-05-06

Name

Mwamengo Ulimboka Baraka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. BARAKA A. U. MWAMENGO aliuliza: -

Je, lini Barabara ya Ipyana – Kasumulu – Ileje itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Baraka Ulimboka Mwamengo, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Ipyana – Kasumulu – Ngana – Ndembo – Ileje eneo la Isongole lenye urefu wa kilometa 114.3 ambapo kwa sasa kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii imefikia 96%. Aidha, Serikali imeanza ujenzi wa barabara hii sehemu ya Isongole II – Ndembo pamoja na barabara ya kuingia Ndembo – Isoko yenye urefu wa kilometa 52 ambapo ujenzi umefikia 10.75%.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sehemu ya Ipyana – Kasumulu – Ngana hadi Ndembo kazi ya kufanya uthamini wa nyumba na mali kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi watakaoathiriwa na mradi huo inategemea kuanza hivi karibuni.