Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 23 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 259 2026-05-06

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. DKT. SELEMANI S. JAFO K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa Barabara ya TAMCO hadi Mapinga utakamilika kwa kiwango cha lami baada ya kusuasua kwa muda mrefu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Barabara ya TAMCO – Mapinga unatekelezwa kwa awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza inahusisha sehemu ya kuanzia NIDA hadi Pangani, kilometa 3.8, na awamu ya pili inahusisha sehemu ya Pangani hadi Mapinga, kilometa 14.62. Ujenzi wa barabara hii unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2027. Aidha, Serikali inaahidi kuipa kipaumbele barabara hii kama sehemu ya kupunguza msongamano kwenye Barabara Kuu ya Dar es Salaam kwenda Morogoro, ahsante.