Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 23 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 260 | 2026-05-06 |
Name
Dr. Christina Christopher Mnzava
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza:-
Je, lini Barabara ya kutoka Old Shinyanga hadi Iselamagazi, Makao Makuu ya Halmashauri ya Shinyanga DC, itajengwa kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Old Shinyanga hadi Iselamagazi yenye urefu wa kilometa 25 ni sehemu ya Barabara ya Salawe – Solwa hadi Old Shinyanga, yenye urefu wa kilometa 80.1. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami imekamilika. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved