Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 23 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 263 | 2026-05-06 |
Name
Kassim Hassan Haji
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwanakwerekwe
Primary Question
MHE. KASSIM HASSAN HAJI aliuliza: -
Je, lini Treni ya Mwendokasi itaanzisha safari za Mchana kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam na kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Kassim Hassan Haji, Mbunge wa Mwanakwerekwe, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania linaendelea kutoa huduma ya usafiri wa treni kila siku kwa njia ya treni Dar es Salaam hadi Dodoma. Aidha, safari za treni kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa siku ni treni nane na safari za treni kutoka Dodoma hadi Dar es salaam kwa siku ni treni nne.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upangaji wa safari za treni unaendelea kuboreshwa ambapo ukamilikaji wa mifumo ya uendeshaji utakapokuwa imefika 100%, shirika litaongeza safari za treni ili kukidhi hitaji kubwa la wateja hasa wateja wetu wanaotoka na kuelekea Zanzibar ili waweze kuunganisha na usafiri wa treni na huduma nyingine za usafiri wanapotoka au kuelekea Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea kuwaomba wateja wetu kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambapo shirika linaendelea na ukamilishaji wa mifumo. Mifumo hii inatarajiwa kukamilika mwanzoni mwa 2026/2027.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved