Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 23 Water and Irrigation Wizara ya Maji 264 2026-05-06

Name

Lutengano George Mwalwiba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. LUTENGANO G. MWALWIBA aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya mapitio ya miradi ya maji Busokelo ili kubaini changamoto kwa baadhi ya miradi kutofanya kazi ipasavyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Lutengano George Mwalwiba, Mbunge wa Jimbo la Busokelo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha mapitio ya awali ya skimu zote 35 zilizopo Jimbo la Busokelo, ambapo skimu 19 zinatoa huduma ya maji ipasavyo wakati skimu 16 zinahitaji ukarabati kutokana na changamoto ya uchakavu wa miundombinu ya muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha uendelevu wa huduma ya maji, Serikali imekamilisha ukarabati wa skimu za maji 12 kati ya 16 zilizobainika kuwa na changamoto ambazo ni Kandete, Lwangwa, Kisegese, Kifunda, Ntapisi, Nswigala, Ikanu, Ipelo, Kalinga, Nyandege, Malyasi na Mpombo ambapo kwa pamoja zimegharimu zaidi ya shilingi bilioni 2.25.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, kupitia bajeti ya 2025/2026 Serikali inaendelea na ukarabati wa skimu ya Kabembe sambamba na upanuzi wa skimu ya Ikanu kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 580.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kufanya mapitio na kukarabati miradi yote yenye changamoto ya uchakavu wa miundombinu nchini ikiwemo ya Jimbo la Busokelo kadiri fedha zinavyopatikana.