Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 23 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 264 | 2026-05-06 |
Name
Lutengano George Mwalwiba
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busokelo
Primary Question
MHE. LUTENGANO G. MWALWIBA aliuliza: -
Je, lini Serikali itafanya mapitio ya miradi ya maji Busokelo ili kubaini changamoto kwa baadhi ya miradi kutofanya kazi ipasavyo?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Lutengano George Mwalwiba, Mbunge wa Jimbo la Busokelo, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha mapitio ya awali ya skimu zote 35 zilizopo Jimbo la Busokelo, ambapo skimu 19 zinatoa huduma ya maji ipasavyo wakati skimu 16 zinahitaji ukarabati kutokana na changamoto ya uchakavu wa miundombinu ya muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha uendelevu wa huduma ya maji, Serikali imekamilisha ukarabati wa skimu za maji 12 kati ya 16 zilizobainika kuwa na changamoto ambazo ni Kandete, Lwangwa, Kisegese, Kifunda, Ntapisi, Nswigala, Ikanu, Ipelo, Kalinga, Nyandege, Malyasi na Mpombo ambapo kwa pamoja zimegharimu zaidi ya shilingi bilioni 2.25.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, kupitia bajeti ya 2025/2026 Serikali inaendelea na ukarabati wa skimu ya Kabembe sambamba na upanuzi wa skimu ya Ikanu kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 580.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kufanya mapitio na kukarabati miradi yote yenye changamoto ya uchakavu wa miundombinu nchini ikiwemo ya Jimbo la Busokelo kadiri fedha zinavyopatikana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved