Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 23 | Community Development, Gender and Children | Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum | 265 | 2026-05-06 |
Name
Janeth Elias Mahawanga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -
Je, kuna mpango gani wa kuanzisha au kuimarisha mifuko maalum ya uwezeshaji kwa wanawake?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Mahawanga kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, inatekeleza mpango madhubuti wa kuimarisha mifuko ya uwezeshaji kiuchumi ukiwemo Mfuko Maalum wa Maendeleo ya Wanawake (Women Development Fund) ambao upo chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum. Mfuko huo unatoa mikopo yenye masharti nafuu kwa wanawake wajasiriamali, iwe ni mtu mmoja mmoja au vikundi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, mkakati endelevu uliopo ni kuimarisha mfuko huo badala ya kuanzisha mifuko mipya sambamba na kuimarisha uwezeshaji wanawake kupitia miradi mbalimbali ya kisekta ya kukopesha wanawake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande mwingine, Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI iko katika hatua za mwisho za kuanza utoaji wa mikopo maalum kwa wanawake kupitia mradi wa pamoja utakaotekelezwa kwa ushirikiano na Benki ya Dunia, hatua itakayoongeza wigo kwa wanawake wengi kunufaika na mikopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuimarisha uwezeshaji wanawake kiuchumi kwa kushirikiana na sekta binafsi, taasisi za fedha na wadau wa maendeleo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved