Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 42 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 504 | 2026-06-03 |
Name
Ester Amos Bulaya
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KANGI A. LUGOLA K.n.y. MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka fedha zilizobaki za utekelezaji wa miradi tisa ya maji yenye thamani ya shilingi bilioni 13 ambapo zimetolewa shilingi bilioni saba tu?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Amos Bulaya, Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa jumla ya miradi nane katika Jimbo la Bunda Mjini, Mkoani Mara kwa gharama ya jumla ya shilingi 21,671,846,983.12 ambapo hadi kufikia sasa jumla ya shilingi bilioni 13.7 zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo. Serikali itaendelea kutoa kipaumbele cha kupeleka fedha za utekelezaji wa miradi hiyo kwa hati ya madai zinazowasilishwa na kadri fedha zinavyopatikana ili iweze kukamilika kwa wakati na ubora stahiki. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved