Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 42 Water and Irrigation Wizara ya Maji 505 2026-06-03

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mradi wa Maji wa Tsoray utakaohudumia vijiji 21 katika Halmashuri ya Mji wa Mbulu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutafuta fedha zaidi ya shilingi bilioni 70 kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Kimkakati wa Tsoray uliopo Tarafa ya Nambis, Wilaya ya Mbulu, Mkoani Manyara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa kazi zinazotarajiwa kutekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji chenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 13.6 kwa siku, ujenzi wa nyumba ya mitambo (pump house), ununuzi na ufungaji wa pampu nne za kusukuma maji, ujenzi wa matanki nane yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 6.6, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 429.5, ujenzi wa vituo 160 vya kuchotea maji sambamba na ujenzi wa mbauti (cattle trough) sita za kunyweshea mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huo ukianza kutekelezwa unatarajiwa kuchukuwa miezi 24 ambapo unalenga kunufaisha zaidi ya wananchi 109,228 waishio kwenye vijiji 21 vya Wilaya ya Mbulu. Ahsante sana.