Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 42 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 506 | 2026-06-03 |
Name
Florent Laurent Kyombo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nkenge
Primary Question
MHE. FROLENT L. KYOMBO aliuliza: -
Je, lini Serikali itatenga bajeti ya kutosha ili kukamilisha ujenzi wa Barabara ya Katoma – Bukwali badala ya kujenga mita 200 kila mwaka?
Name
Abdallah Hamis Ulega
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkuranga
Answer
WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Missenyi kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea na ujenzi wa Barabara ya Katoma – Bukwali kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa jumla ya kilometa 8.2 kati ya kilometa 39.83 zimejengwa kwa kiwango cha lami. Kwa sehemu iliyobaki kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina inaendelea na imefikia 65%. Baada ya usanifu kukamilika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved