Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 42 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 507 2026-06-03

Name

Silvery Luboja Salvatory

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:

Je, lini upanuzi wa barabara kuu kwa njia nne kutoka Kenyatta – Usagara Mwanza utaanza?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Silvery Luboja Salvatory, Mbunge wa Misungwi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya upanuzi wa Barabara ya Mwanza Mjini hadi Usagara imekamilika ambapo itahusisha urefu wa kilometa 25 kutoka njia mbili zilizopo sasa kwenda njia nne. Kwa sasa utaratibu wa manunuzi wa kumpata mkandarasi wa ujenzi wa barabara unaendelea. Kazi ya ujenzi itaanza mara moja baada ya mkandarasi kuwa amepatikana, naomba kuwasilisha.