Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benjamin Lukubha Ngayiwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kahama Mjini

Primary Question

MHE. BENJAMIN L. NGAYIWA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuipandisha hadhi Hospitali ya Manispaa ya Kahama kuwa Hospitali ya Rufaa?

Supplementary Question 1

MHE. BENJAMIN L. NGAYIWA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali kuhusu kuboresha huduma katika hospitali yetu ya Manispaa ya Kahama, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; Mheshimiwa Naibu Waziri amesema Serikali inatenga bajeti kwa ajiili ya kuboresha huduma kwa kujenga jengo la dharura na kuweka vifaa vya uchunguzi kwa maana ya CT- Scan. Sasa ni lini Serikali ina mpango wa kupeleka CT- Scan kwenye hospitali hii ambayo inapokea wagonjwa wengi sana kutoka hospitali zingine?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ni lini sasa Serikali ina mpango wa kuboresha na kukamilisha majengo ya zahanati ambayo yamefikia hatua za lenta kama vile Chalya, Nyandekwa na sehemu zingine za Wilaya yetu? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ngayiwa. Kwanza, ninampongeza Mjumbe wa Kamati ya TAMISEMI anatoa michango mizuri kwa ajili ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kweli kwa idadi kubwa ya wagonjwa ambao tunawapokea katika hospitali hii ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama na uhitaji wa CT- Scan kwa ajili ya upimaji, uchunguzi wa mifupa kwa wagonjwa wetu, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa maana ya kwamba ndani ya muda mfupi Serikali imekwishafanya tathmini na uhitaji huo tumeshauona, tunaipeleka CT-Scan pale ili iende kutoa matibabu kuwahudumia wahitaji wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu zahanati nilikwishaeleza hapa kwamba zaidi ya zahanati 1,841 zinakwenda kufanyiwa ukarabati na kumaliziwa maboma, Serikali inajielekeza zaidi katika miradi hii ambayo tayari imekwishaanzishwa ili tuweze kuikamilisha kabla ya kuanza miradi mingine ya zahati na vituo vya afya. (Makofi)

Name

John John Nchimbi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. BENJAMIN L. NGAYIWA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuipandisha hadhi Hospitali ya Manispaa ya Kahama kuwa Hospitali ya Rufaa?

Supplementary Question 2

MHE. JOHN J. NCHIMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, Kata yangu ya Mpepo katika Wilaya ya Nyasa ndiyo kata ya pili kwa ukubwa katika Wilaya yangu. Kwa bahati nzuri inapakana na nchi ya jirani ambapo mwaka jana ilisababisha maambukizi ya ugonjwa wa M-Pox kutoka katika nchi ya jirani, lakini kata hiyo mpaka sasa pamoja na unyeti wake haina kituo cha afya. Nini kauli ya Serikali ili kulinda maisha ya wananchi wa Nyasa kutokana na njia hiyo ambayo imeonekana inapitisha magonjwa mengi na bado hakuna sehemu ya afya ya kuwalinda wananchi wangu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa John John Nchimbi, Mbunge wa Nyasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Serikali inaendelea kupambana na haya magonjwa ya mlipuko, kupitia vile vituo vya kimkakati Mheshimiwa Mbunge ataweza kutuambia kama kituo hicho kiende kikajengwe katika kata hii, yeye mwenyewe atatupa uelekeo huo na tutaona namna gani ya kwenda kuboresha katika kituo chetu cha afya hicho na tunaweza tukajenga kituo cha kimkakati katika Jimbo hilo.