Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Isack Joseph Copriano
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Monduli
Primary Question
MHE. ISACK J. COPRIANO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha Mradi wa Maji wa Vijiji 13 vya Jimbo la Monduli?
Supplementary Question 1
MHE. ISACK J. COPRIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali dogo la nyongeza. Unajua fika Wilaya ya Monduli kwa sasa ni kame na ukizingatia mabwawa yote yamekwisha maji na wananchi wa Monduli wanapata maji Arusha. Je, Waziri haoni sasa ni wakati muafaka wa Serikali kuiangalia Monduli kwa jicho la huruma ili wananchi wale wapate huduma ya maji? (Makofi)
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Isack Joseph.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Kaka yangu, nilifanya ziara katika Jimbo la Monduli mwaka jana na mwaka juzi akiwa Diwani na tuliweza kutembelea miradi mingi ikiwemo na bwawa lililokuwa linajengwa na tukachukua hatua kwa wakandarasi ambao walikuwa wanaleta uzembe katika utekelezaji wa miradi ndani ya Monduli.
Mheshimiwa Naibu Spika, upatikanaji pia wa huduma ya maji katika Wilaya ya Monduli na Jimbo la Monduli ni 77% mpaka sasa ambapo miradi zaidi ya mitano imekamilika yenye gharama ya shilingi bilioni 3.4 na kuna miradi mingine inayoendelea takribani miradi 10 yenye gharama ya shilingi bilioni 41 ambayo Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alituelekeza Wizara ya Maji kuhakikisha kwamba tunazipeleka Monduli.
Mheshimiwa Naibu Spika, huu mradi ambao unaendelea sasa ambao umefikia 15% wenye gharama ya shilingi bilioni 20.3. Kwa hiyo, tunaamini kabisa katika uwekezaji huu ndani ya Jimbo la Monduli miradi hii itakapokamilika, ongezeko la upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wa Monduli hautakuwa na changamoto yoyote. Ninakushukuru sana. (Makofi)
Name
Sara Msafiri Ally
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Mvomero
Primary Question
MHE. ISACK J. COPRIANO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha Mradi wa Maji wa Vijiji 13 vya Jimbo la Monduli?
Supplementary Question 2
MHE. SARA M. ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongea. Jimbo la Mvomero lina miradi sita ya maji inayoendelea ambayo imekuwa ikisuasua kutokana na changamoto za kifedha ikiwepo Mradi wa Maji wa Tandale - Homboza na Mradi wa Dakawa. Je, lini Serikali itapeleka fedha ili hii miradi sita ikamilike kwa wakati na wananchi waweze kupata huduma? (Makofi)
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la nyongeza la dada yangu Mheshimiwa Sara Msafiri, Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nilifanya ziara kwenye Jimbo la Mvomero na Mradi huu wa Dakawa pamoja na Tandale ni kweli kabisa kwamba ni mkombozi kwa wananchi wa Mvomero utakapokamilika, lakini kati ya miradi ambayo 878 inayoendelea yenye gharama ya shilingi trilioni 1.3 na hii miradi iko humu. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha miradi viporo vyote inaisha ili wananchi waweze kuona matokeo na maji yatoke kwa ajili ya matumizi ya maji safi na salama. Ninakushukuru sana. (Makofi)
Name
Joshua Samwel Nassari
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Arumeru-Mashariki
Primary Question
MHE. ISACK J. COPRIANO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha Mradi wa Maji wa Vijiji 13 vya Jimbo la Monduli?
Supplementary Question 3
MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru. Nitumie nafasi hii kuipongeza kwanza Wizara ya Maji kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya kwenye majimbo yetu huko, lakini nina swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Uwilo pale Arumeru pamoja na Mradi mkubwa wa Maji wa Embaseni - Kikatiti pale Arumeru, ni lini Serikali itapeleka fedha ili wakandarasi waweze kurudi site na miradi hii iweze kuendelea kwa sababu tayari ilikwishaanza lakini imesimama?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Nassari, Mbunge wa Arumeru, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Nassari kwa kazi kubwa ambayo anaendelea kuifanya, lakini kubwa zaidi ushirikiano wake na Wizara ya Maji katika kubainisha changamoto zinazotokea katika jimbo lake. Tunamhakikishia kwamba, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan itapeleka fedha ili kuhakikisha miradi hii inakamilika na iweze kutoa matokeo na wananchi waweze kuona maji kwenye bomba hatimaye sasa nchi yetu isiwe na tatizo la water stress. Kwa hiyo, tunamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, hilo tunalichukua kwa makini sana. Ahsante sana.
Name
Joseph Kasheku Musukuma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Geita
Primary Question
MHE. ISACK J. COPRIANO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha Mradi wa Maji wa Vijiji 13 vya Jimbo la Monduli?
Supplementary Question 4
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji ulioko katika Kata ya Rwazera ni mradi ambao ni tegemezi kwa Kata ya Kamwanga, Bugalama, Isulwabutundwe, lakini ujenzi wa mradi huu unasuasua sana, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kwenda nami kuuona huo mradi ili wasukume pesa ukamilike?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasheku Musukuma kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Mheshimiwa Kasheku Musukuma ameendelea kuwasiliana na Wizara ya Maji na ameendelea kuwasiliana na Mheshimiwa Waziri kuhakikisha kwamba tunachukua hatua katika mradi huu. Sasa kwa ombi lake hili mahsusi kwa Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Musukuma kwenda katika jimbo lake na kuangalia.
Name
Jafari Wambura Chege
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Rorya
Primary Question
MHE. ISACK J. COPRIANO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha Mradi wa Maji wa Vijiji 13 vya Jimbo la Monduli?
Supplementary Question 5
MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi. Nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina swali la nyongeza. Mradi wa Maji wa Miji 28 Rorya, Tarime umesimama kwa muda mrefu na Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana nami mradi ule umekwenda kwa kusuasua sana kwa muda mrefu kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa mradi huo.
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Mradi huu wa kutoka Tarime – Rorya ambao awali tulitegemea mradi huu pia ukatoe huduma maeneo ya Serengeti, Mugumu kule ni kweli umesuasusa. Hata hivyo, Wizara tumechukua hatua ya kukaa na Wakandarasi wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha. Mradi huu Mkandarasi aendelee kuutekeleza ili lengo ni kwamba atakapokuwa ana-raise certificate, basi Serikali itaweza kumlipa kulingana na kazi atakayokuwa ameifanya. Ninakushukuru sana.