Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. Yahaya Esmail Nawanda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nanyumbu
Primary Question
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA aliuliza:- Je, lini Barabara za Chikalule hadi Lihanga na Lochinu hadi Mkwiti zitajengwa?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; Mfuko wa Barabara umekuwa unagharamia zile barabara ambazo ziko rasmi na umekuwa unajenga Barabara kutoka Mkoma Sokoni hadi Lihanga. Je, ni lini sasa Serikali itatenga fedha maalum kwa ajili ya kumalizia sasa kutoka Lihanga mpaka Chikalule, ambayo ni kama kilometa moja?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Barabara ya Mchemo hadi Mahuta imekuwa ina changamoto kubwa sana. Je, ni lini Serikali sasa itapandisha hadhi ya barabara hii kutoka udongo kwenda kutengenezwa kuwa barabara changarawe ili wananchi wa maeneo haya waweze kupita kwa usalama?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, ninatambua kuwa jiografia ya Mji wa Newala Vijijini ina miinuko mikali na barabara hii ambayo imetajwa na Mheshimiwa Mbunge, Barabara ya Chikalule kwenda Makao Makuu ya Kitangali wananchi wetu kwenye maeneo yale wakati mwingine wamelazimika kupitia Lindi ili kufika makao makuu ya wilaya. Kwa kutambua umuhimu huo pia zipo taasisi kwenye eneo hilo, ikiwemo Shule yetu ya Msingi Chikalule ambayo inafanya vizuri sana; na ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya wananchi wale.
Mheshimiwa Spika, Serikali itakwenda kuijenga barabara hii kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Tumepanga, kwenye Mwaka wa Fedha unaofuata wa 2026/2027 tutaweka fedha kwa ajili ya barabara hii.
Mheshimiwa Spika, siyo hivyo tu, kwenye swali lake la pili ameitaja Barabara ya Mchemu hadi Mahuta na Mheshimiwa Nape wakati ameanza kuuliza alitaka kuitaja barabara hii. Tunatambua kuwa barabara hii imebeba uchumi mkubwa wa zao la korosho kwenye maeneo ya Newala pamoja na Tandahimba na ina urefu wa kilometa 17.
Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha ujao ninawaelekeza mkoa waiangalie barabara hii vizuri ili waihuishe kwenye mipango yetu ya kitaifa na hatimaye iweze kujengwa na kuinua uchumi na kufungua uchumi wa Wananewala pamoja na Wanatandaimba.
Name
Nape Moses Nnauye
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtama
Primary Question
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA aliuliza:- Je, lini Barabara za Chikalule hadi Lihanga na Lochinu hadi Mkwiti zitajengwa?
Supplementary Question 2
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Hoja yangu ya msingi ilikuwa ni kwamba hii Barabara ya kutoka Mtama kwenda Newala Vijijini hadi Newala Mjini kama nilivyosema ni barabara kubwa ya uchumi mkubwa na inaunganisha mikoa miwili, Mtwara na Lindi na wilaya zetu. Barabara hii imekuwa ikijengwa kidogo kidogo sana, yaani fedha inatoka kidogo kidogo sana. Ni wakati sasa Serikali iamue kutoa fedha kuimaliza badala ya kuwa inajenga hivi kidogo kidogo na uchumi wetu unaendelea kudorora kwenye eneo hili husika.
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, tunatambua umuhimu wa barabara hii. Kama nilivyotangulia kusema, barabara hizi tutazitengea fedha kwenye mipango yetu. Kwenye eneo hili si barabara hiyo tu yenye umuhimu, ipo Barabara ya kutoka Maputi kwenda Ndanda, pia iko Barabara ya kutoka Chiwonga, Pacha Nne hadi Nanganga njia panda ya kwenda Ruangwa. Zote hizi ni barabara tunazozitazama kwa jicho la ukaribu na tutakwenda kuhakikisha kwamba barabara hizi zinafunguka. Ni dhamira ya Mheshimiwa Rais kuhakikisha kwamba uchumi unafunguliwa, barabara zinafunguliwa.
Name
Moses Ludovico Kaegele
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nkasi Kusini
Primary Question
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA aliuliza:- Je, lini Barabara za Chikalule hadi Lihanga na Lochinu hadi Mkwiti zitajengwa?
Supplementary Question 3
MHE. MOSES L. KAEGELE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana. Kijiji cha Tundu ni kijiji chenye wakazi zaidi ya 3000 na kijiji hicho kipo pembezoni mwa Ziwa Tanganyika, namna pekee ya kufikia pale kijijini ni njia ya maji. Tokea ziwa limechafuka wakazi wa pale hawafikiki. Je, ni lini serikali itatenga fedha kwa ajili ya kufungua Barabara kutoka Kala kwenda Tundu na kujenga madaraja mawili ili wananchi hawa waweze kupata huduma za msingi kwa wakati?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, ninaomba nikiri kuwa Mheshimiwa Mbunge alikwishakuja ofisini kwenye ofisi zetu za TAMISEMI. Tumekwishakaa na watalam, tumeangalia umuhimu wa barabara hii ambayo ipo pembezoni kabisa, lakini inaenda kwenye kata yenye wakazi zaidi ya 3000. Kupitia mradi wetu wa Mheshimiwa RISE tunaangalia uwezekano wa kuweka madaraja; ambapo yanahitajika madaraja takribani matatu; ili tuweze kufungua uchumi kwa eneo lile na kusaidia wananchi wetu wa eneo lile.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved