Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Edward Olelekaita Kisau
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kiteto
Primary Question
MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini mnara wa Redio Tanzania uliojengwa Kiteto utaanza kufanya kazi?
Supplementary Question 1
MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Niipongeze Serikali kwa majibu mazuri, mafupi, safi. Sasa swali dogo tu la nyongeza. Kwa siku ambazo si nyingi sana ni lini upo tayari ututembelee Kiteto ili kuweza ku-monitor mradi huu muhimu sana kwa wananchi wa Kiteto?
Name
Hamis Mohamed Mwinjuma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muheza
Answer
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa zuri la nyongeza la Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Kiteto na nimpongeze kwa kazi kubwa anayoifanya kuwapigania Wanakiteto. Hili la kuambatana naye kwenda Kiteto wala siyo suala la mjadala, atakapokuwa tayari Mheshimiwa Mbunge anifahamishe tujadiliane kuhusiana na ratiba ya Bunge na shughuli nyingine za Serikali, tufunge safari kwa ajili ya kwenda Kiteto.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved