Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. Yahaya Esmail Nawanda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nanyumbu
Primary Question
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA aliuliza:- Je, lini Mradi wa Maji wa Makonde utakamilika?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Mradi wa Makonde ni mradi mkubwa sana ambao Serikali imekubali yenyewe kwa kusema jumla ya watu 600,000 wanakwenda kunufaika katika Wilaya za Newala, Tandahimba pamoja na Mtwara. Hivi tunapozungumza mkandarasi hayupo site, na alishawasilisha certificate za madai ya jumla bilioni 11.2. Je, ni Serikali italipa fedha hizo ili mkandarasi aendelee na shughuli yake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika mradi huo wa Makonde kuna miradi miwili pacha, Mradi wa Lukohe pamoja na Mradi wa Malatu, miradi hii yote kandarasi CTC Construction Company amefanya kazi na amewasilisha jumla ya certificate tatu zenye jumla ya shilingi 6,000,000,000 na hayupo site. Je, Serikali ina kauli gani ya kuhakikisha mkandarasi anarudi ili miradi hii iweze kukamilika?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Yahya Esmail Nawanda, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa na nzuri ambayo anaendelea kuifanya katika jimbo la Newala Vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri kabisa, kwamba mradi huu kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema, ni mradi mkubwa na ni wa kimkakati. Asili yake ni mradi uliojengwa mwaka 1954, ambapo ukarabati wake ulianza mwaka 2022. Kuna zaidi ya matenki manne ambayo yatajengwa Newala Mjini, Newala Vijijini, Tandahimba pamoja na Nanyamba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu tayari fedha ambazo mkandarasi ameshalipwa zaidi ya bilioni 20.7 ambapo mradi umefikia 40% kama ambavyo nimejibu katika jibu la msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu pia kwamba, mkandarasi anadai takribani bilioni 10.8 ambazo tayari zipo kwenye mchakato na zitakapokamilika mkandarasi atalipwa, ambaye ni ECC. Tunaamini kwamba mradi huu unatakiwa ukamilike na wananchi wapate huduma ya maji safi na salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mradi wa pili ambapo mkandarasi pia naye anadai; kama ambavyo nilijibu hapa kuwa uwepo wa madai ya wakandarasi ni ishara tosha kwamba Serikali ina dhamira ya kweli kuhakikisha kwamba inatatua changamoto za wananchi na ndiyo maana tumeamua kuwekeza miradi mingi ili kuhakikisha kwamba wananchi wanatatuliwa changamoto zao, wakiwemo wananchi wa Newala Vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe hofu, hizi bilioni sita tutahakikisha kwamba mkandarasi analipwa ili arudi site na kuhakikisha kwamba anaendelea na mradi na kuukamilisha kwa wakati, ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved