Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Patali Shida Patali
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbeya Vijijini
Primary Question
MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza: - Je, lini Miradi ya Maji ya Tuwemacho, Masuguru-Mchoteka, Liwanga, Msinji na Azimio itakamilika?
Supplementary Question 1
MHE. PATALI S. PATALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa mwaka wa fedha uliopita na mwaka wa fedha huu unaoendelea Serikali imekuwa ikitekeleza miradi sita Jimbo la Mbeya Vijijini ambayo ni Mradi wa Maji Zira, Mbagara - Yunga Mradi wa Maji wa Masoko Mradi wa Maji wa Ilea pale Ihango, Mradi wa Maji wa Ranje, Tembela pamoja na Mradi wa Maji wa Kisima, Isuto. Miradi hii imesimama kutokana na wakandarasi kukosa fedha za kuendelea na miradi hii.
Je, ni lini Serikali itawalipa wakandarasi hawa ili wakandarasi warejee site kutekeleza miradi hii Wanambeya Vijijini wapate maji? Ahsante.
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Patali Patali, Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kipaumbele cha Serikali kwa sasa ni kuhakikisha kwamba tunamalizia miradi yote ya maji ambayo inaendelea na hivi sasa tuna miradi 1206 ambayo inaendelea kote nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa Mheshimiwa Patali Patali ambaye nakumbuka nikiwa katika ziara alikuja kushiriki katika mradi ule wa Kiwira ambapo tunatambua kwamba ushirikiano wa Mbeya yote na ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba tunaendelea kutekeleza na utekelezaji na kuanzishwa kwa miradi hii ya 1206 ni ishara tosha ya dhamira ya kweli ya Serikali ya kuhakikisha inaleta huduma ya maji safi na salama na toshelevu kwa Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wakandarasi kuendelea kulipwa tumeshakwisha weka mkakati kuanza kuwalipa awamu kwa awamu kulingana na vipaumbele vya maeneo husika, lengo ni kwamba tukitekeleza mmoja ukakamilika ukatoa matokeo basi tunakuja na mradi mwingine. Hatuwezi kuipeleka miradi yote kwa pamoja ikakamilika kwa pamoja, lazima mkakati wetu sasa Waheshimiwa Wabunge tuelewe kwamba tumekubaliana tuweke awamu kwa awamu ili Wabunge wote waweze kuguswa katika maeneo yao, tusije tukajikuta tunapeleka fedha zote katika miradi yote katika eneo moja na eneo lingine likakosa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge wa Mbeya Vijijini tutakupatia vipaumbele ambavyo tumeviweka katika mkakati wetu na wewe utashiriki kushauri ili tuone namna gani tutafanya vizuri zaidi kwa ajili ya wananchi wako wa Mbeya Vijijini. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved