Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Canute Joachim

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CATHERINE C. JOACHIM aliuliza: - Je, Serikali imepata matokeo gani katika kupunguza uchafuzi wa mazingira tangu kuanza kwa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki mwaka 2019?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CATHERINE C. JOACHIM: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kuainisha mafanikio ambayo yamepatikana katika udhibiti wa taka za plastiki. Nina maswali mawili ya nyongeza ambayo yatajikita katika eneo namba nne, lililosemwa na Mheshimiwa Naibu Waziri, kuhusiana na gharama za kupunguza udhibiti wa taka za plastiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza. Kwa kuwa miundombinu ya kukusanyia takataka pamoja na vile vituo vya urejelezaji wa taka za plastiki ni vichache, je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza miundombinu hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili litajikita katika ongezeko la viwanda, ambalo tumeona linakwenda sambamba na ongezeko la vifungashio vya plastiki pamoja na chupa ambazo hutumika mara moja. Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti ongezeko hili la vifungashio vinavyotumika mara moja bila kuathiri ukuaji wa viwanda hapa nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Catherine Joachim, Mbunge anayetokana na Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi. Ninatambua kwamba Jumuiya ya Wazazi moja ya kipaumbele chake ni kulinda na kuhifadhi mazingira.

Mheshimiwa Naibu Spika, maswali yake ya nyongeza ninaomba niyajibu yote kwa pamoja. Sheria yetu ya Mazingira Sura 191, tuliitungia kanuni Kifungu kile cha 230, kifungu cha 2(f). Kanuni zile ndiyo zilihusu haya makatazo ya matumizi ya mifuko ya plastiki na hususan vifungashio vya plastiki, kwa kutambua umuhimu wa sekta za kilimo ambazo zina mahitaji makubwa ya matumizi ya plastiki, vilevile sekta za ujenzi ambazo zina matumizi makubwa ya mahitaji ya plastiki, sekta za vyakula kwa maana ya vifungashio, viwandani kama alivyotangulia kusema Mheshimiwa Mbunge, lakini vilevile sekta za afya, pamoja na kwenye usimamizi wa taka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kanuni zile ambazo tulizitunga chini ya kifungu hicho cha Sheria ya 230, ziliweza kuruhusu maeneo haya baadhi ya wazalishaji kupewa kibali kwa ajili ya kuzalisha plastiki hizo kwa matumizi hayo ambayo ni muhimu ndani ya uchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ambacho tumekifanya kama Serikali kwenye kanuni zile ambazo tumezitunga, tumeweka pia na wajibu wa wazalishaji wa plastiki hizo, wasafirishaji, wanaohifadhi, wanaosambaza na wanaotumia, tumewapa wajibu wa kuhakikisha pia wanashiriki kwenye kukusanya na kuteketeza taka hizo ambazo zinakuwa zimetokana na bidhaa ambazo wamehusika nazo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeendelea kuimarisha pia miundombinu ya ukusanyaji wa taka hizi. Sheria ile ambayo tuliitunga, Sheria ya Mazingira Sura 191 imezipa Mamlaka za Serikali za Mitaa jukumu la kusimamia taka ngumu. Kwa hiyo, kwa kushirikiana na Mamlaka za Serikali za Mitaa, pia tunahakikisha pana miundombinu kila mahali, kwenye miji yetu na kwenye majiji yetu kwa ajili ya uhifadhi wa taka hizi ngumu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.

Name

Josephine Joseph Kapoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CATHERINE C. JOACHIM aliuliza: - Je, Serikali imepata matokeo gani katika kupunguza uchafuzi wa mazingira tangu kuanza kwa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki mwaka 2019?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. KAPOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa ninataka niulize swali dogo la nyongeza. Nchi nyingi kwa sasa zimeshapiga hatua kubwa sana katika kubadilisha taka kuwa fursa za kibiashara. Je, Serikali ina mkakati gani wa kujielekeza katika mlengo huu ili kutokomeza hili suala la uchafuzi wa mazingira? (Makofi)

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza sana Mbunge wa Mkoa wa Morogoro kwa swali lake zuri, na amekuwa msemaji mzuri sana kuutetea Mkoa wa Morogoro pamoja na Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuweka jitihada kubwa katika kuhakikisha kwamba taka zinazozalishwa kwenye mazingira ya shughuli zetu za kiuchumi kwenye miji yetu, kwenye majiji na maeneo mbalimbali zinakuwa recycled, yaani zinarudishwa kutumika kwa ajili ya kuzalisha bidhaa ambazo zitatumika tena kwenye mzunguko wa uzalishaji kwenye maeneo mbalimbali ya kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, Serikali inahakikisha kwenye majiji makubwa, mathalan kama ilivyo Dar es Salaam inajenga madampo makubwa na ambayo yataambatana na miundombinu ya viwanda vitakavyoendelea kufanya recycling, yaani marejeo na marejesho ya hizo taka ili ziweze kutumika tena kwa ajili ya kuzalisha bidhaa zitakazotumika kwenye maeneo yetu.