Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Chacha Mwita Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CHACHA M. WAMBURA aliuliza:- Je, upi mkakati wa kuunda ajira na kukuza uchumi wa vijana kupitia miradi ya uzalishaji na ujasiriamali ili kupunguza utegemezi wa sekta ya madini – Geita?

Supplementary Question 1

MHE. CHACHA M. WAMBURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, tunajua kwamba uchumi wa Geita unategemea sana sekta ya madini na nia ni kuhakikisha kwamba tunapata miradi mbadala ambayo tutakuwa hatutegemei madini tu. Kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambapo uchaguzi ulifanyika mwaka 2025 ilionesha kwamba tunaenda kupata miradi ambayo itaenda kukuza ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni kwa ajili ya uhakika kwamba vijana wanapata ajira na wanaenda kukua kiuchumi. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga hii miradi ili hao vijana wa Geita waweze kupata sehemu ya kufanya kazi na kupata ajira? (Makofi)

Name

Rahma Riyadh Kisuo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali zuri la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Chacha Wambura, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imepokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge wa kuanzisha miradi mikubwa ya kimkakati ili kuzalisha ajira na fursa mbalimbali kwa vijana wa Mkoa wa Geita. Ninataka nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge, Serikali iko tayari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, ningependa pia kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kwamba uanzishwaji wa miradi mikubwa na ya kimkakati unategemea bajeti ya Serikali iliyotengwa. Hivyo basi, Mheshimiwa Mbunge ushauri wake umepokelewa na utafanyiwa kazi kadiri bajeti ya Serikali itakavyoruhusu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.