Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Tarimba Gulam Abbas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kinondoni
Primary Question
MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, kwa nini Serikali haitoi bei elekezi kwa makato ya huduma za Mobile Money ili kuwapunguzia gharama wananchi?
Supplementary Question 1
MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaipongeza Serikali kwa hatua ambazo inazichukua katika kuhakikisha kwamba utumiaji wa huduma za kidijitali kwenye utumiaji wa fedha unakuwa na unafuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu mimi lililenga kwenye huduma ya simu kwa simu, sikuwa na tatizo kati ya benki na simu, simu na benki, lakini ni mtu kwa mtu. Simu moja kwenda simu nyingine. Ukituma unakatwa fedha, ukipokea unakatwa fedha; mwananchi hana unafuu. Swali langu ni kwa nini kusiwepo na bei elekezi kutoka Benki Kuu kuweka kikomo kama ilivyoweka kikomo kwenye huduma za benki na simu? Hilo ni swali la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Ni kwa nini Serikali isifikirie kuondoa angalau upande mmoja, kwamba ukituma unaweza ukakatwa, lakini wakati wa kupokea, wapokee bure, ili fedha ziweze zikazunguka na kuwasaidia wananchi wetu kuwaondolea mzigo? Ahsante sana. (Makofi)
Name
Amb. Khamis Mussa Omar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nominated
Answer
WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema, ninamshukuru sana Mheshimiwa Tarimba Abbas, kwenye swali lake na ni kweli kulikuwa na sehemu muhimu hii ambayo ameitaja ya huduma ya fedha za moja kwa moja, mtu na mtu. Kwenye hili ndiyo nilisema kwamba sera yetu hasa ilikuwa ni kuendelea kuwa na soko huria, lakini kwa kujali masilahi ya mlaji. Kwa sasa hivi hakukuwa na bei kwenye ukomo wa bei, lakini Benki Kuu imeendelea kufuatilia kwa ukaribu gharama ambazo zinatumika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Benki Kuu imeendelea kutoa mwongozo; na imetoa mwongozo wa ada hizi ambazo zinatozwa na kampuni za simu kwenye huduma za mobile service, imetoa mwongozo mwaka 2024, imesisitiza kuwepo kwa uwazi na disclosure. Kwa hiyo, kila mtoa huduma za malipo ya fedha analazimika kuweka bei ambazo atazi-charge ambazo tunazitumia kwenye huduma za kutuma na kutolea pesa.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Benki Kuu imeweka kiwango cha ulinganisho, kimeweka kwenye portal, na pia imeweka na kiwango cha ulinganisho, wenyewe wanaita plus comparator ambayo inasaidia watumaji na watoaji wa huduma kuweza kuona zile charge zenyewe. Kwa hiyo, kwenye ukomo hakujawekwa, lakini kumetolewa mwongozo wa namna ya kuweka chargers mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili la Mheshimiwa Tarimba lile la kuondoa upande mmoja, tulichukuwe, lakini kwa sasa hivi bado mtumaji na mtoaji vilevile wanachajiwa kwa sababu wote wawili wanapata huduma.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved