Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Cosmas Mtesigwa Bulala
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwimba
Primary Question
MHE. COSMAS M. BULALA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao katika Kijiji cha Hungumalwa?
Supplementary Question 1
MHE. COSMAS M. BULALA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Hungumalwa Jimbo la Kwimba ni kitovu cha biashara ya ukusanyaji, usafirishaji na usambazaji wa mazao kwenye Mkoa wa Mwanza ambao unategemewa na wilaya jirani za Kishapu, Shinyanga Vijijini, Misungwi, Magu na Shinyanga Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini hasa tathmini hiyo itafanyika na kukamilika; na kwa sababu tayari wananchi wa Kijiji cha Hungumalwa wameshatenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa ghala ili utekelezaji wa mradi huo uanze?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Wiki iliyopita kumetokea janga katika Vijiji vya Buyogo na Mwang’ombe kwenye Kata ya Hungumalwa ambapo mvua kali ya mawe imenyesha na kuharibu mazao kama mtama, viazi pamoja na mpunga uliopo mashambani. Je, Serikali ina mpango gani wa dharura kwenda kusaidia wananchi walioathirika na mafuriko haya? (Makofi)
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza Mheshimiwa Cosmas Bulala, Mbunge wa Jimbo la Kwimba, kwanza, kwa maswali yake ya msingi, na pili, kwa ufuatiliaji ambao amekuwa akiufanya muda wote.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo maja, tunatambua umuhimu wa Mji wa Hungumalwa na tunatambua biashara kubwa inayofanyika pale na nimthibitishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika mwaka wa fedha huu tunaokwenda kuuanza, Serikali itafanya tathmini katika eneo hilo. Baada ya tathmini, tutatafuta fedha ambayo nimhakikishie kwamba tutajenga ghala ambalo litawasaidia wananchi wake katika eneo la Hungumalwa ambao wapo katika Jimbo la Kwimba. Kwa hilo, nina uhakika nalo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu changamoto ambayo imetokana na mvua, nimwambie tu kwamba Wizara ya Kilimo tutashirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ambao ndio wana jukumu kubwa la kuratibu maafa na wakati wanafanya ule uratibu, kila Wizara ina jukumu lake. Kwa hiyo, tukishamaliza jukumu hilo ninaamini Serikali chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan itapeleka msaada katika eneo hilo kwa wananchi ambao wamekutwa na maafa hayo, ahsante sana.
Name
Athumin Omary Mapalilo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. COSMAS M. BULALA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao katika Kijiji cha Hungumalwa?
Supplementary Question 2
MHE. ATHUMIN O. MAPALILO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Wanawake wa Mkoa wa Mtwara hujihusisha zaidi na kilimo cha kunde, njugu na karanga, je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza mazao haya katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani ili tuwe na uhakika wa soko? (Makofi)
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nimpongeze vilevile Mheshimiwa Mbunge kwa swali la msingi. Ni kweli stakabathi za ghala imekuwa na faida kubwa kwa wananchi, na tumekuwa tukiingiza zao moja baada ya linguine, maana yake hatuwezi kuingiza mazao yote kwa wakati mmoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunaangalia vilevile na ukubwa wa biashara ya hayo mazao, lakini na upatikanaji wake kwa urahisi, na biashara ya soko husika. Kwa hiyo, tutalifanyia tathmini zao la kunde ili tufanye haraka iwezekanavyo kuingiza katika Mfumo wa Stakabadhi ya Ghala.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili maana yake tunafanya sisi Wizara ya Kilimo tukishirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara ambao ndiyo wasimamizi wa Bodi ya WRRB wale wasimamizi wa stakabadhi ya ghala.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved